Wednesday, June 25, 2014

MWANAMKE sudan aliyeachiwa huru atuhumiwa kwa kughushi nyaraka za safari


Bi Merian Ibrahim akiwa na Mumewe

MWANASHERIA  wa mwanamke wa Sudan aliyekamatwa siku chache baada ya kuhukumiwa kifo kwa kuasi dini ya Kiislam kwa kuolewa na Mkristo, amesema mteja wake anatuhumiwa kwa kughushi nyaraka za safari.


Amesema mwanamke huyo Meriam Ibrahim bado anashikiliwa katika kituo cha polisi katika mji Mkuu wa Khartoum.Sudan Kusini ambayo ndio iliyompa nyaraka hizo imesema kuwa nyaraka hizo ni halali kwa vile ameolewa na mwanaume raia halisi wa Sudan Kusini.

Mwanasheria wa Meriam Ibrahim amesema yeye pamoja na mumewe walikuwa wakiohojiwa kuhusuana na hati za kusafiria. Ilikuwa inasadikiwa kuwa walikuwa wanasafiri kuelekea nchini Marekani.

Awali Marekani ilisema itashirikana na Sudan kuhakikisha kuwa mwanamke aliyesamehewa hukumu ya kifo kwa kuasi dini ya Kiislam anaruhusiwa kuondoka nchini humo baada ya kukamatwa katika uwanja wa ndege wa Khartoum.

Mwanamke huyo Meriam Ibrahim, alihukumiwa kifo kwa kosa la kuolewa na mwanamume mkristo na kukana dini ya kiisilamu alikamatwa akiwa na familia yake katika uwanja wa ndege mjini Khartoum.


No comments:

Post a Comment