Wednesday, June 25, 2014

HATIMAE wafanyakazi wa mgodi wa dhahabu nyeupe warudi kazini


Wachimbaji wa dhahabu nyeupe Afrika kusini

MAELFU ya wafanyakazi wa migodi ya dhahabu nyeupe nchini Afrika kusini wamerudi kazini kufuatia makubaliano ya malipo yao ya miaka mitatu ya kumaliza mgomo ambao umedumu kwa muda wa miezi mitano.


Baada ya kutokuwa kazini kwa muda mrefu wafanyakazi hao watapewa mafunzo na kufanyiwa ukagauzi wa kiafya nahuenda ikachukua miezi kadha kabla ya shughhuli kwenye migodi kurejelea hali ya kawaida.

Mgomo huo unakisiwa kugharimu makampuni hasara ya dola bilioni mbili na kusababasha kudorora kwa uchumi wa afrika kusini.

Chama cha wafanyakazi hao cha AMCU kilitia sahihi mapatano mbalimbali na kampuni za Lonmin, Impala na Anglo American hiyo yana.

Wafanyakazi hao hawakupata mshahara waliotarajia wa Rand za Afrika Kusini 12,500 (zaidi ya Dola 1,000) lakini walikubali mkataba wa miaka mitatu ambapo wataendelea kuongezwa mshahara, penisheni, malipo ya nyumba na bima ya Afya.

Tayari wafanyakazi hao wamerudi kazini katika machimbo hayo ya dhahabu nyeupe hii leo lakini ni dhahiri kuwa itachukua miezi kadhaa kabla ya uzalishaji wa madini hayo kufikia hali yake ya kawaida.

Mkataba huo wa miaka mitatu uliotiwa sahihi pamoja na kampuni za Lonmin, Impala Platinum na American Platinum imemaliza mgomo mrefu zaidi kuwahi kutokea nchini Afrika Kusini na ambao umegharimu taifa pesa nyingi sana.

Wazalishaji wa dhahabu nyeupe walipata hasara ya Dola Bilioni 2 na wafanyakazi hao wakapoteza mishahara ya Dola Bilioni moja tangu mgomo huo uanze Januari mwaka huu.



No comments:

Post a Comment