Monday, July 21, 2014

MANISPAA ya Morogoro yatenga sh. milioni 168 kwaajili ya ujenzi wa kituo cha afya


Mbunge wa Morogoro mjini Abdulaziz Mohamed Abood

HALMASHAURI ya Manispaa ya Morogoro imetenga shilingi mil.168 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya cha kata ya Mafisa ikiwa ni kuunga mkono juhudi nguvu kazi za wananchi waliojitolea kufanikisha hatua za awali za ujenzi huo.


Diwani wa kata ya Mafisa,Francis Kayenzi alibainisha hayo mwishoni mwa wiki kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika mtaa wa Mafisa.

Katika mkutano huo diwani Kayenzi alisema katika bajeti ya halmashauri hiyo ya miaka miwili shilingi Mi.168 zimeelekezwa kituoni hapo kukamilisha ujenzi huo na kuwaondolea adha wanachi ya kutembea umbali mrefu kusafa huduma hiyo.
Hata hivyo akihamasisha michango zaidi,alisema baada ya kukamilika kwa jengo hilo upo mpango wa kujenga nyumba za wahudumu wakiwemo madakitari na wauguzi kama kivutio kwa wataalamu hao kwenye kata hiyo.
 


Katika mkutano huo Diwani huyo alianisha jinsi fedha hizo zilivyopatikana akimtaja mbunge wa jimbo Abdulaziz Abood aliyetoa shilingi Mil.3.6 na yeye kujitoa shilingi Mil.1.200,000.
 



















No comments:

Post a Comment