Monday, July 21, 2014

MAPIGANO yaendelea Sudan Kusini



UMOJA  wa mataifa umesema kumekuwepo kwa siku mbili za mapigano katika mji wa Nasir, Sudani ya Kusini.

Msemaji wa Umoja wa matifa amesema vikosi vya waasi vimeyakalia maeneo ya katikati ya mji huo ambao mapema mwaka huu ulitumika kama makao makuu ya muda ya kiongozi wa waasi Riek Machar.
Shirika la Habari la Reuters linaripoti kuwa kambi ya waasi wa Sudani Kusini imesema inatuma ujumbe Ujumbe wake kuelekea nchini Uganda kufanya mazungumzo na Rais Yoweri Kaguta Museveni ili kumwomba Museveni kuondoa vikosi vyake vya kijeshi katika Sudani Kusini ambako vilipelekwa kuisaidia serikali ya Juba.
Mwezi Januari Rais Museveni alisema vikosi vyake vinamuunga mkono rais wa Sudan Salva Kiir dhidi ya waasi wanaoongozwa na aliyekuwa makamu wa rais Riek Machar.

No comments:

Post a Comment