Saturday, July 26, 2014

UPANUZI wa kituo cha Ifakara waanza


Wauguzi wa hospitali Saint Francis Ifakara

UPANUZI wa kituo cha afya Kibaoni wilayani Kilombero kuwa Hospitali umeanza kwa kuongeza miundombinu ukitaraji kutumia zaidi ya shilingi Bil.1.012  kutokana na mapato ya ndani na nje mwaka huu katika halamashauri hiyo.


Upanuzi huo unaofanyika kwa awamu mbili unaotaraji kuwanufaisha zaidi ya wanachi 500,000 kwa mwaka wakiwemo wakazi na wageni wilayani humo ulianza katika mwaka wa fedha 2010/11 ukitaraji kukamilika 2014/15.

Mganga mkuu wa wilaya Dk Tom Mtoi alimwambia mwandishi wa habari hizi kuwa kukamilika kwa mradi hua utakao wanufaisha moja kwa moja zaidi ya wakazi 407,880 unaokwenda sambamba na ongezeko la watumishi,vifaa tiba,madawa na chumba cha kuhifadhi maiti.
.
Mganga huyo mkuu alisema ujenzi wa majengo hayo umetekelezwa na mkandarasi na hadi sasa ujenzi wa chumba cha upasuaji umekamilika na kinatumika na wodi 2,chumba cha kuhifadhia maiti na jingo la mionzi vimekamilika huku ujenzi wa wodi 3 unaendelea katika hatua ya awali na linta.
Kuhusu changamoto Dk.Mtoi alibainisha upungufu wa watumishi wenye sifa kukidhi ikama ya hospitali akifafanua kuwa kituo kina jumla watumishi 77 kati ya 206 watakaokidhi utoaji huduma ya afya hospiltalini hapo .








No comments:

Post a Comment