Wednesday, November 5, 2014

MAMILIONI ya waislamu Ulimwenguni washiriki siku ya Ashura


Waislamu wakiwa katika siku ya ASHURA

MAMILIONI  ya Waislamu kote duniani wanashiriki katika hafla za maombolezo ya Siku ya Ashura, ambayo hufanyika kwa mnasaba wa kukumbuka kuuawa shahidi Mjukuu wa Mtume Muhammad SAW, Imam Hussein AS pamoja na wafuasi wake huko Karbala.

Mamilioni ya waombolezaji katika Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na nchi zingine duniani wamejitokeza mitaani, misikitini na kumbi za kidini maarufu kama Husseiniya kwa ajili ya kukumbuka Siku ya Ashura, ambayo ni siku ya 10 ya Mwezi Mtukufu wa Muharram.
Waumini kote Iran wamesimamisha sala ya jamaa wakati wa adhuhuri kukumbuka namna Imam Hussein AS pamoja na mashahidi wengine wa Karbala walivyosimamisha sala ya jamaa kwa wakati pamoja na kuwa katika hali ngumu ya vita.

No comments:

Post a Comment