Wednesday, November 5, 2014

SUA kuanza kuzalisha wasomi wabunifu


CHUO Kikuu cha kilimo cha Sokoine cha Morogoro

MRADI wa tafiti bunifu za kilimo (AGRI) unaofadhiliwa na shirika la misaada la Marekani (USAID) ikishirikiana na chuo kikuu cha Sokine cha kilimo (SUA) na wizara ya kilimo chakula na Ushirika umeanza safari ya kuzalisha wasomi wataalamu wabunifu 135 nchini watakao kabiliana na changamoto za kilimo kupitia bunifu zao katika sekta hiyo na lishe.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi wa Mradi huo kutoka Marekani Profesa David Kraybill na Msaidizi wake kutoka SUA Profesa Issac Minde walipozungumza na waandishi wa habari katika ofisi za MOROPC mjini hapa.
Katika

Mradi unalenga kuzalisha wataalamu katika ubunifu huo kati yao nusu wakiwa wanawake, kufanya tafiti za kisayansi katika bara la Afrika,Amerika ya kasikazini na Asia,kukifanya SUA kuwa chuo cha usalama wa chakula nchini na kuimarisha uhusiano baina ya Tanzania,Mrekani na nyingine katika katika masuala hayo.
“vyuo vikuu vya marekani kikiwemo cha Michigan, Ohio,Virginia Tec,Tuskegee,Florida na chuo kikuu cha lowa Stete tayri vimezalisha wasomi 67 wakiwemo 51 wa sahahada ya uzamili,16 shahada ya uzamivu”alisema
Katika fafanuzi zake aliongeza kuwa wanachuo 30 vyuo vya Afrika kikiwemo SUA-Tanzania,Makerere-Uganda,Lilongwe-Malawi,Nairobi,Kenyatta,Jomo Kinyata,Egerton vya Kenya,Stellenbosch cha Afrika ya kusini na chuo kikuu cha Zambia”Aliongeza
Profesa Kraybill alisema mbali na vyo hivyo wanafunzi 35 wakiwemo 10 wa shahada ya kwanza na wawili sahada ya uzamimivu walihitimu mafunzo yao chuo kikuu cha SUA na wanafunzi sita wako chuo kikuu cha Punjab nchini India.
Kwa upande wake Profesa Minde mbali na kupongeza mafanikioa makubwa tafiti zilizo zalishwa,iAGRI pia imekiwezesha chuo kuimarisha njia za ufunshaji,kusaidia upatikanaji tafiti,SUA kuwa na mahusiano mazuri na yenye tija kwa chuo,mhitimu na jamii.



No comments:

Post a Comment