Wakulima wa mbogamboga Kilosa, Morogoro |
WAKULIMA wa mbogamboga na viungo wilayani
Kilosa wameiomba
serikali,taasisi,makampuni na watu binafsi nchini kote
kujitokeza kuwekeza katika kuongeza thamani,ufungaji bora na
kuyawezesha mazao hayo kudumu kwa muda mrefu ili wanufaike
nayo.
serikali,taasisi,makampuni na watu binafsi nchini kote
kujitokeza kuwekeza katika kuongeza thamani,ufungaji bora na
kuyawezesha mazao hayo kudumu kwa muda mrefu ili wanufaike
nayo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti kwenye ziara ya mafunzo
iliyoandaliwa na Halmashauri hiyo na mashirika ya kiraia
ikiwemo Mviwata,Ibrahim Mlima na Nasibu Hussen walisema
wanaomba viwanda hivyo ili wanufaike na kilimo hicho ambacho
kwa sasa kimefikia zaidi ya asilimia 50 ya wanachozalisha
kuharibikia shamba.
Walisema ziara hiyo iliyowakutanisha wakulima wa kijiji cha
Kibunga ,Ulaya na Mbuyuni wilayani humo katika bustani za
kijiji cha Ibingu imewafumbua macho baada ya kubaini kuwa
mazao mengi ya wazalishaji nchini yanaharibikia shamba kwa
kukosa viwanda kama hivyo.
Awali afisa kilimo kutoka mtandao wa wakulima wadogo nchini
Mviwata Amanzi Amanzi aliwataka wasomi nchini kuanza kuni
njia zitakazofanikisha kutegua changamoto ya upotevu wa
mazao mashambani ili yawanufaishe wakulima amabao wengi wao
huishia kubaki na madeni baada ya kuzalisha.
Aidha aliwataka maafisa ugani kutekeleza kwa vitendo kazi na
fani waliyosomea kwa kuwa karibu na wakulima hususani
katika kipindi hiki cha kuelekea utayarishaji wa mashamba
hadi kuvuna ili wazalishe kwa tija.
No comments:
Post a Comment