Thursday, November 6, 2014

RAIA wa China wadaiwa kukutwa kutoroshwa na meno


Rais wa China Xi Jinping

INADAIWA kuwa wanunuzi, raia wa Uchina walinunua maelfu ya kilo za pembe za ndovu nchini Tanzania na kuzitorosha kutoka nchini humo katika ndege ya kibinafsi ya raia wa Uchina Xi Jinping,wakati alipozuru bara Afrika.

Kulingana na shirika la ujasusi la mazingira lililo na makao yake mjini London.
Pembe hizo zilinunuliwa wiki moja tu kabla ya ziara ya rais huyo wa Uchina nchini tanzania mwaka ulioipita ambapo zilifichwa katika mifuko ya wanadiplomasia ili kutokamatwa.
Pembe za ndovu
Shirika hilo pia linadai kwamba wajumbe waliokuwa wakiandamana na Rais Xi walinunua viwango vikubwa vya pembe hizo.

No comments:

Post a Comment