Thursday, November 6, 2014

WAFANYAKAZI nchini Mali wapatiwa chanjo ya Ebola


Wauguzi wakiwa kazini

KUNDI  la wafanyakazi wa afya nchini Mali leo wanapewa chanjo ya majaribio dhidi ya ugonjwa wa Ebola.

Hii ina maana kwamba watu waliojitolea kufanyiwa chanjo ya majaribio nchini Mali kufikia watu 40.
Utafiti ulianza Mali kufuatia majaribio salama kufanyika nchini Uingereza na Marekani.
Chanjo hiyo imetengenezwa na wanasayansi katika Taasisi ya Taifa ya Mzio na Magonjwa ya Kuambukiza huko Maryland, nchini Marekani na inatengenezwa na kampuni ya dawa ya Uingereza ya GlaxoSmithKline

No comments:

Post a Comment