![]() |
Wanakikundi wa mkaa Endelevu wakiwa kazini |
KONGAMANO la mkaa
Endelevu limemalizika na kukubaliana kuwa mradi wa mkaa Endelevu uendelee
wilayani Kilosa mkoa wa Morogoro.
Akifunga kongamano hilo mwishoni mwa wiki, mjini Kilosa, Mkuu wa
wilaya ya Kilosa Eliasi Tarimo ambaye alikuwa mwenyekiti wa kongamano
alihitimisha kwa kuruhusu kuendelea kwa mradi huo kwa masharti ya kuchagua miti
inayofaa kwa mkaa(selective)na si kukata miti yote (clear felling)kwani ni hatari kwa uahi na usalama wa miti.
Mradi wa mkaa Endelevu unafanyika wilayani Kilosa ukiwa ni
majaribio , unaendeshwa na Taasisi ya uhifadhi wa Misitu(TFCG), kwa kushirikia na Mjumita wakifadhiliwa na
serikali ya Uswisi.
Wataalamu bobezi wa misitu toka Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine
cha Morogoro wakiongozwa na mtaalamu Nguli masuala ya Misitu Profesa Romanus
Ishengoma wasilisha mada mbalimbali juu ya faida na madhara ya ukataji miti
sanjari na urasimishaji wa biashara ya mkaa nchini.
No comments:
Post a Comment