![]() |
Wananchi wa Yeman wakiwa katika maandamano |
Hii ni katika hali ambayo kwa mujibu wa
shirika hilo, jeshi la Misri nalo linajiandaa kuingia kijeshi nchini Yemen kwa
kisingizio cha kulinda lango la Babul-Mandab. Kwa mujibu wa AP, hali ya hatari
imetanda nchini Yemen kufuatia hatua ya Wamagharibi kuwaondoa wanadiplomasia
wake nchini humo siku ya Jumatano, na kusisitiza kuwa hivi sasa Riyadh
inayapatia silaha na zana na kivita makabila yaishio katika maeneo ya kusini
mwa Yemen.
Aidha AP
imewanukuu viongozi wa ngazi za juu nchini Yemen ambao hawakutaka kutaja majina
yao, wakieleza kuwepo njama za pamoja kati ya Saudia na Misri kwa lengo la
kuanzisha mashambulizi kwa uungaji mkono wa Marekani dhidi ya Yemen. Imefafanua
zaidi kwamba, Saudia imekuwa ikituma silaha kwa makabila ya mkoa wa Ma'rib katika
kipindi chote cha mgogoro wa kisiasa nchini humo.
No comments:
Post a Comment