![]() |
Viongozi wa Red Arrow wakiwa na viongozi wa TFF |
Uongozi wa klabu hiyo chini ya mwenyekiti wake Col Nolacso K Chilando ulifika makao makuu ya Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Tanzania - TFF sambamba na Afisa habari wa klabu Lt Col Melody Siisii, Bw Alex Chila ofisa ubalozi wa Zambia nchini Tanzania kujitambulisha uwepo wao nchini.
Wakiongea na katibu mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Tanzania - TFF Selestine Mwesigwa, uongozi wa timu hiyo umesema maandalizi ya kambi yamekamilika na kikubwa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini Tanzania watambue uwepo wao na kuwasaidia kupata viwanja vya kufanyia mazoezi.
Naye Katibu Mkuu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini -TFF Mwesigwa alisema wameyapokea maombi hayo ya Red Arrow FC na kuwakaribisha nchini kwa ajili ya kambi yao na kusema ujio wao utafungua milango kwa vilabu vingine pia kuweka kambi Tanzania.
No comments:
Post a Comment