Monday, February 16, 2015

SHAHIDI kesi ya Ponda akana kusikia maneno ya uchochezi toka kwa Sheikh Ponda



Sheikh Ponda akiwa  mahakamani

SHAHIDI wa nane G 1293 DC Abdalah dhidi ya kesi ya katibu wa Jumuia ya waislamu Ponda Issa Ponda amekana kumsikia mtuhumiwa akitoa maneno yoyote ya uchochezi dhidi ya dini nyingine.


Akito ushahidi mbele ya hakimu mfawidhi mkazi Marry Moyo Asikari huyo wa idara ya upelelezi mkoa alisema mbali na siku ya tukio kupewa kazi ya kurekodi mhadhara wa shehe Ponda hakusikia neno lolote ambalo lingesababisha athari katika imani nyingine.

Alisema mbali na kazi hiyo hakuwahi kusikia mlio wowte wa mlipuko katika eneo la tukio wala Shehe Ponda kupigwa risasi hadi mwisho wa mhadhara huo.
“Baada ya kurekodi nilifikisha kwa mkuu wangu kisha kurudisha nyuma kazi niliyorekodi kumwonyesha mkuu wangu wa kazi kisha niliigunga na kumkabidhi vifaa vya kurekodia ikiwemo kamera”alisema G1293 wakati akihojiwa na wakili wa utetezi Juma Nasoro akisaidiwa na Abubakar Salim.

Hata hivyo akiongozwa na wakili wa mashitaka   Bernard Kongola akisaidiana na George Balasa shahidi huyo aliithibitishia mahakama kuwa kilichorekodiwa kwenye kamera hiyo ni sahihi na kuitaka mahakama kukiamini kwakua kamera haiwezi kupoteza kumbukumbu kama ilivyo kwa mwanadamu.
“kilichorekodiwa ni sahihi kwakua hiki ni chombo ambacho hakiwezi kupoteza kumbukumbu tofauti na binadamu ambae anaweza kusaweza kusahau au kuchanganya taarifa”alifafanua shahidi G1293 na kukabidhi kama kielelezo mahakamani hapo.

Baada ya shahidi kukamilisha ushahidi wake,wakili wa mashitaka Bernard Kongola aliiomba mahakama kuahilishwa shauri hilo hadi Februari 26 watakapomleta shahidi wa tisa na wa mwisho kati ya 15 waliotaraji kuwaleta dhiidi ya shitaka hilo ombi lililokubaliwa na pande zote na kesi kuahilishwa.
Baada ya kuahilishwa kwa mahakama hiyo wakili wa utetezi Juma Nasoro aliwaambia waandishi kuwa uamuzi wa mashitaka kupunguza mashahidi ni ishara njema kwa mteja wao kuendelea kutaabika na unawaonyesha upande wa mashitaka hawana ushahidi wa kuntia hatiani mteja wao.
“kwa mujibu wa sheria hatua inayofuata baada ya washitaki kufunga ushahidi tutakwenda katika hatua ya pili kuona kama mshitakiwa anakesi ya kujibu au laa…kwa upande wetu mpaka sasa hatuoni ambapo Ponda anabanwa na sheria kama alivyoshitakiwa”alisema Nasoro
Alisema kwa mujibu washitaka nikuwa mteja wao anashitakiwa kwa kutoa maneno ya kuumiza hisia ya dini nyingine na pili kuhamamsisha waislamu kufanya mkutano usio halali ambapo mpaka sasa hakuna shahidi hata mmoja aliyeshuhudia Ponda kutoa ushahidi huo.
“kwa mtazamo wetu mpaka sasa Ponda hana kosa maana hakuna aliyethibitisha kuumizwa kwa dini nyingine badala yake mashahidi wanachanganyana wakisema waislamu mara wakristo wengine wapani na hakuna pia aliethibitisha Ponda kushawishi mkutano usio halali…wameleta ‘clip’ ya video hapa nayo hakuna sehemu Ponda akisikika kutamka maneno kulingana na kosa lilivyo”alifafanua
Hakimu mfawidhi mkazi Marry Moyo aliahilisha shauri hilo hadi Februari 26 mwaka huu ambapo upande wa mashitaka unataraji kufunga ushahidi wake kwa kumleta shahidi wake wa Tisa na kumpatia nafasi hakimu kutafsiri sheria endapo shehe Ponda anakosa la kujibu au laa.

No comments:

Post a Comment