Monday, February 16, 2015

KIPINDI cha Dira ya Mazingira kusikika wilayani Kilosa




MBIU ya Maendeleo Media Group kuendesha kipindi cha  Dira ya Mazingira katika  redio  jamii wilayani Kilosa mkoa wa Morogoro.

Mhariri mkuu wa  Mbiu ya Maendeleo Media Group na Msimamizi mkuu wa kipindi cha Dira ya Mazingira Bi Salma Mlamila ameeeleza hayo mwishoni mwa juma wakati akiongea na wadau wa mazingira  wilayani Kilosa kwa njia  ya simu.
 
Kipindi hicho kitaanza kurushwa rasmi februari 16, mwaka huu katika kituo cha Radio Jamiii kinachomilikiwa na Halmashauri ya wilaya ya Kilosa, mkoani Morogoro.


Kwa takribani wiki mbili kipindi hicho kitagusa sekta ya Misitu na kitakuwa kikizungumzia jitihada za wakala wa Huduma za  misitu nchini(TFS)katika kutunza, kusimamia na kuhifadhi misitu na siku ya jumatatu kitakuwa kikimuhoji Meneja wakla wa misitu wilaya ya Kilosa Bwana  John Olomi.
 
Bi Salma Mlamila amewataka wadau mbalimbali wa mazingira kukiunga mkono kipindi hicho kwa kushiriki kupitia kipindi hicho cha siku ya Jumatatu na jumanne saaa tatu na nusu usiku.
Ameeleza  kuwa, makala za vipindi hivyo zitakuwa zikipatikana katika blog  ya Mbiua ya Maendeleo ambayo ni www.mbiuyamaendeleo.blogspot.com

No comments:

Post a Comment