Sunday, March 29, 2015

MBUNGE azinasihi Taasisi za dini kuhamasisha amani


Mheshimiwa Abdul Azizi Abood akiongea na wananchi

MBUNGE wa jimbo la Morogoro AbdulAziz Abood ameonyesha hofu ya machafuko katika uchaguzi ujao na kuziangukia Taasisi za dini mkoani humo akizitaka kuimarisha maombi ya amani na utulivu ili tuvuke salama na kuendeleza maisha.

Akihutubia kwenye kongamano la kuchangia vifaa vya kanisa la Tanzania Assemblies o God viwandani mjini humo,Abood aliwashauri waumini na viongozi wa dini vijembe na fitina kuwaachia wanasiasa majukwaani.

“jamani vurugu tuisikie kwa wenzetu tu katika nchi jiarani lakini janga hilo lisitukute,wanaoumia na kufa kama nzige waliopulizwa dawa ni wanawake na watoto ambao ni warithi wa Taifa hili baadae…jamani kwenye vita hakuna kula,kusali wala kukaa sehemu mkacheka kila mtu ni adui yako”alisisitiza Abood.

Mbali na salamu hizo kwa taasisi za dini,mbunge huyo amewataka wanaolitaka jimbo hilo kujitokeza kushindana nae  na kuvisihi vyama vya siasa kuwaandaa wagombea wao kisikolojia ili waendeshe kapeni za kitaaluma pasipo kushawishika kufanya vurugu ambazo hatima yake ni machafuko.
“nimebakiza wastani wa miezi mitatu kumaliza ngwe yangu kwa mujibu wa katiba niliyoapa pale Dodoma na mimi nirudi tena kuwaomba ridhaa nyingine ya kuwatumikia…nimzisikia nia na wengine wanajinadi kuwa sinta rudi,leo nawaanbieni kuwa kwa mapenzi yake mungu nitarudi tena”alifafanua.
Alitaja baadhi ya mambo makubwa yaliyokuwa yakimuumiza kichwa na kukosa usingizi kabla hajaingia katika nafasi hiyo kuwa ni pamoja kuziba mianya ya wizi wa fedha za umma katika halamashuri ya manispaa,kuboresha huduma ikiwemo muindombinu kama barabara,maji,majengo na kuwainua walalahoi kwa mitaji na maeneo ya kufanyia kazi.
Awali akimkaribisha kuzungumza na waumini wa kanisa hilo,Mchungaji kiongozi Sauli Magawa aliemuunga mkono mbunge huyo kwa kutangaza kurejea tena kwenye nafasi hiyo alisema kanisa hilo lenye madhumuni ya kukomesha uovu kwa jamii,kuelimisha na kukemea maadili linakabiliwa na upungufu wa vifaa mbalimbali zikiwemo spika,visemeo visivyounganishwa na waya,kinanda na busta.
“vyote nilivyokutajia vinathamani ya shilingi Mil 3,500,000  na tunaimani kuwa Mungu atatutangulia na kuvipata kupitia wadau wa maendeleo ukiwemo wewe…umewasikia waumi wanavyokusihi kuwania tena tunakuongeza nguvu ya kushawishika ufanye hivyo”alifafanua Magawa.
Hata hivyo Abood alichangia shilingi 500,000 na kuwasihi kutosita kumwalika hata kama hatakuwa ameshinda katika uchaguzi ujao akidai hiyo ni dhamira yake tangu hajafikiria kuwania nafasi hiyo.


No comments:

Post a Comment