Friday, July 24, 2015

BALOZI sefu Iddi kuwa mgeni rasmi Kilosa , mkoani Morogoro



Balozi Seifu Alli Iddi
MAKAMU wa pili wa Rais serikali ya mapinduzi Zanzibar Balozi Seif Alli Iddi  Julai 24 anataraji kuwa mgeni rasimi katika maadhimisho ya siku ya idadi ya watu Duniani itakayofanyika kitaifa Wilayani Kilosa mkoani Morogoro.

 Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake, Mkuu wa mkoa wa Morogoro Dk Rajabu Rutengwe alisema maadhimisho hayo yenye kauli mbiu 'watu waliokatika mazingira hatarishi wakati wa dharura' yanafanyika kwa mara ya pili mkoani hapa hususani wilayani Kilosa kutokana na wilaya hiyo kukumbwa na majanga ya kibinadamu na mazingira yakiwemo Mafuriko.

"niheshima kubwa kwa mkoa wetu kufanyika maadhimisho haya kwa mara ya pili ikizingatiwa mwaka 2012 yalifanyika Manspaa ya Morogoro kwakua ianautangaza mkoa, lakini safari hii yatafanyika wilayani Kilosa hasa kutokana na wilaya hii kukumbwa sana na majanga ya kibinadamu na mazingira kama mafuriko"alifafanua Dk Retengwe.

Alisema maadhimisho hayo yatakayotanguliwa na matukio matatu likiwemo la jana Julai 22 ambapo umoja wa vijana wa umoja wa Mataifa YUNA kuwakutanisha zaidi ya vijana 200 wenye kati ya umri wa miaka 15-30 katika viwanja vya Karimjee jijini Dar es salaam.

Tukio lingine ni maonesho na utoaji huduma kwa jamii ikiwemo uzazi wa mpango,elimu ya huduma ya kwanza katika majanga na uandikishaji vyeti vya kuzaliwa sambamba na na kutembelea wanachi majumbani kutoa elimu hiyo kwa siku tatu wilayani kilosa.

Maadhimisho haya yalianza kufanyika mwaka 1990 ambapo yamekuwa yakiadhimishwa kila 11 Julai ya mwaka ikilenga kuhamasisha watu kuelewa umuhimu wa takwimu ya watu na Maendeleo na inakadiriwa karibu watu Mil.60 duniani hususani wanake na watoto katika mwaka 2014 hawakuwa na makazi kwa majanga





No comments:

Post a Comment