Friday, July 24, 2015

TAHA yaombwa kuwasaidia wakulima wa bilinganya



CHAMA cha wataalamu na wakulima wa mbogamboga nchini (TAHA) kimeombwa kuboresha na kukuza zao la bilinganya ili kuwawezesha wakulima wa zao hilo kuondoka na umaskini wa kipato.


Ushauri huo umetolewa hivi karibuni na wakulima wa mbogamboga wilayani Korogwe mkoa  wa Tanga wakati wakiongea na Mbiu ya maendeleo wilayani humo.

Wanapongeza hatua za kuanzishwa kwa chama hicho nchini kikiwa na lengo la kuwakomboa wakulima wadogo wadogo, lakini wanapaswa kutambua kuwa wakulimawa mazao ya mbogamboga wanahitaji msaada wa taaluma sanjari na ule wa masoko.

Wameeleza kuwa, soko la uhakika na mbinu bora za uzalishaji wa  bilinganya inayomudu ushindani wa soko ndiyo changamoto kubwa kwao

No comments:

Post a Comment