WATU
watatu wameripotiwa kuuawa katika machafuko
yanayoendelea nchini Burundi.
Taarifa zinaeleza kuwa, watu hao
wameuawa katika machafuko yaliyoibuka kuanzia Jumamosi na kuendelea jijini
Bujumbura baina ya jeshi la polisi na wapinzani wa serikali ya Rais Pierre
Nkurunziza wa nchi hiyo.
Kwa mujibu wa habari, watu wengine
kadhaa wamejeruhiwa wakiwamo polisi wawili, huku idadi kadhaa ya wapinzani
wengine wakitiwa mbaroni. Wakati huo huo jeshi la polisi jijini Bujumbura
limekadhibisha habari ya kuuawa mwandishi wa habari wakati akitekeleza majukumu
yake katika machafuko hayo na kusema kuwa, habari hiyo haina ukweli wowote ule.

No comments:
Post a Comment