Ufadhili huo mpya umewezeshwa na
uamuzi usio wa kawaida wa Bodi ya Benki ya Dunia kutoa misingi ya ufadhili
iliyotengewa nchi za kipato cha chini pekee, na umefanywa wakati Rais wa Benki
ya Dunia akiwa ziarani na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Lebanon.
Katika makubaliano hayo, ambayo
ni sehemu ya Benki ya Dunia kuzisaidia Lebanon na Jordan kufuatia ukarimu wao
kwa kuwapa hifadhi wakimbizi wa Syria, fedha hizo zitasaidia kuboresha viwango
vya mfumo wa elimu wa Lebanon ambao sasa unakabiliwa na shinikizo kubwa, pamoja
na kusaidia katika kupanua upatikanaji wa elimu kwa watoto wote wa Syria wenye
umri kati ya miaka mitatu na 18.(Kwas ihsan ya Redio ya UM )

No comments:
Post a Comment