![]() |
| Rais wa Iran Hassan Rouhan |
RAIS Hassan
Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Iran iko tayari kuimarisha
uhusiano wake na Pakistan katika nyuga zote.
Rais
Rouhani amesema hayo mbele ya waandishi wa habari katika siku ya mwisho ya
ziara yake nchini Pakistan na kuongeza kuwa, Iran imejiandaa vilivyo kutekeleza
vizuri makubaliano yake na Pakistan kama vile kuiuzia gesi nchi hiyo licha ya
kuweko vizuizi vingi ikitaraji kuwa Pakistan nayo itatekeleza vilivyo ahadi
zake katika suala zima la kumalizia utengenezaji wa bomba la kusafirishia gesi
ya Iran kuelekea nchini humo.
Rais wa
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekumbushia umuhimu wa bandari ya Chabahar (kusini
mashariki mwa Iran) na bandari ya Gwadar (kusini magharibi mwa Pakistan) na
kuongeza kuwa, iwapo bandari hizi mbili zitaunganishwa vizuri, basi zitakuwa ni
kituo muhimu sana cha kuziunganisha nchi zote za Asia Mashariki kama vile
China.
Rais wa
Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amerejea hapa nchini baada ya kumaliza ziara ya
siku mbili nchini Pakistan ambako ameonana na Rais, Waziri Mkuu, mshauri wa
Waziri Mkuu katika masuala ya kigeni wa nchi hiyo pamoja na kushiriki katika
kikao cha pamoja cha kiuchumi cha wafanyabiashara wa Iran na Pakistan na
kuhudhuria sherehe za kutiwa saini hati sita za ushirikiano katika nyuga
tofauti.(kwa Ihsan ya Irib )

No comments:
Post a Comment