WATU wasiopungua 12 wamepoteza
maisha Algeria kufuatia ajali ya helikopta wakati ikilinda doria katika eneo la
jangwa la Sahara nchini humo.
Wizara ya Ulinzi ya
Algeria imetoa taarifa na kusema helikopta hiyo ilianguka Jumapili kutokana na
matatizo ya kiufundi.
Taarifa hiyo imefafanua
kuwa tukio hilo lilijiri wakati
helikopta hiyo ilipokuwa ikiruka baina ya miji ya Adrar na Reggan katika eneo
la Tamanrasset.
Uchunguzi umeanzishwa na
jeshi la nchi hiyo kuhusu ajali hiyo.
Algeria imekuwa
ikipambana na magaidi wa Kitakfiri hasa kundi la kigaidi la Al Qaeda katika
eneo la Maghreb AQIM.
Jumapili iliyopita,
jeshi la Algeria liliua magaidi wanne na kuwajeruhi wengine watatu katika eneo
la jangwani wakati magaidi hao waliposhambulia kituo cha kuzalisha gesi.

No comments:
Post a Comment