Tuesday, March 29, 2016

DONALD Trump ashitakiwa kwa kumshambulia mwandishi wa habari

Donald Trump
MENEJA wa kampeni ya urais nchini Marekani kupitia tiketi ya chama cha Republican Donald Trump , ameshtakiwa kwa kumshambulia mwandishi wa habari katika mkutano wa kampeni.

Bwana Corey Lewandowski ameshtakiwa kwa shambulio dhidi ya aliyekuwa mwandishi wa Breitbart Michelle Fields.
Mnamo tarehe 8 mwezi Machi Bwana Lewandowski alimvuta na kumuangusha chini alipojaribu kuuliza swali na kujeruhiwa mkono.

Bwana Lewandowski anapanga kukana shtaka hilo,ilisema timu ya kampeni za bwana Trump

No comments:

Post a Comment