Thursday, March 24, 2016

Dr Shein aahidi kupambana na watakao vunja amani Zanzibar

Rais wa Zanzibar Dr Ali Mohamed Shein 
RAIS wa Zanzibar Ali Mohamed Shein ameapa kupambana na utovu wa usalama katika kisiwa hicho.

Shein ambaye aliapishwa leo baada ya kushinda uchaguzi wa marudio uliosusiwa na upinzani amesema kuwa atafanya kila awezalo kuzima majaribio yeyote ya kuitumbukiza kisiwa hicho katika uhasama.
Shein alitangazwa mshindi wa asili mia 90% ya kura zote zilizopigwa Jumapili iliyopita.
Uchaguzi huo wa marudio uliitishwa baada ya kura iliyopigwa mwezi Oktoba mwaka uliopita kufutiliwa mbali baada ya kiongozi wa upinzani alidai kushinda.




No comments:

Post a Comment