Thursday, March 24, 2016

MKURUGENZI apokelewa kwa mabango

MKURUGENZI na mwenyekiti wa  Halmashauri ya wilaya Morogoro wapokelewa kwa mabango  toka kata mpya ya Kibuko, makao makuu ya Halmashauri ya wilaya hiyo, Mvuha Morogoro vijijini .


Baadhi ya kero zilizoinishwa baada ya kuibuliwa na wanachi katani humo kwa ushirikiano na Mtandao wa jinsia nchini TGNP ni pamoja na kata hiyo kutelekezwa bila huduma za kijamii zikiwemo shule,kituo cha afya,maji safi na salama,maafa yatokanayo na migogoro ya wakulima na wafugaji.

Katika risala yao iliyosomwa na Latifa Hussen mbele ya kaimu mkurugenzi Ernest Khisombi na kaimu mwenyekiti wa halmashauri hiyo Emilly Kidevu wanachi hao walisema mbali na kusongwa na changamoto hapo juu kunajipu la uwekezaji uchwara wasio na manufaa nao bdalayake unawasababishia maafa na maumivu kutokana na milipuko ya baruti zitumikazo  mgodini hapo.
“hizi ni baadhi ya kero zinazotukera kwa muda mrefu na kuja kwetu hapa ni kupata majibu ya hatima yake nini na sisi tutanufaikaje na changamoto hizo ikiwemo ya kutokuwa na huduma hata moja za kijamii sambamba na mgodi uliopo Mwalazi unamanufaa gani kwetu…tunaomba majibu “alisema Latifa.
Alisema kata hiyo mpya kutoka kata mama ya Mkuyuni imetelekezwa baada ya kujigawa na kuwaachia nawanchi mzigo mkubwausio na msaada kwao hasa juu ya ujenzi wa miundombinu ya huduma za kijamii na kutokuwepo kwa faida ya uwekezaji katika mgodi huo wa madini.







No comments:

Post a Comment