Thursday, May 12, 2016

SUKARI Moro yagoma kushuka bei



BEI ya sukari Mkoani Morogoro imeendelea kuwa kitendawili kwa mlaji kutokana na kushindikana kushuka kulingana na bei elekezi ya serikali iliyotolewa na Waziri Mkuu Majaliwa Kasim aliyoitoa karibuni kwenye Bunge la Jamuhuri ya muungano wa Tanzania linaloendelea Mjini Dodoma.


Uchunguzi uliofanywa na mwandishi wa habari hizi mkoani Morogoro umebaini bei hiyo inashindikana kushuka kutokana na bei ya jumla kungangania kwenye bei ya shilingi 96,000 kwa mfuko wa sukari wenye uzani wa kilo 50.
“unajua ndugu yangu hapa serikali inajichanganya yenywe,fikiria sukari leo tumenunua mfuko wa kilo 50 shilingi 96,000 yaani kila kilo moja ni shilingi 1,920 hivi ukiuza shilingi 1,800 faida yako iko wapi ni afadhali waseme tuwe tunagawa bure ndio maana tunauza angalau shilingi 2000”alisema Kasim Maulidi mfanya biashara wa duka Kihonda.
Alisema serikali inaweza kujipanga kukabiliana na changamoto ya upungufu wa sukari kwa kuruhusu sukari toka nje kuingia huku ikirekebisha kodi na ushuru kwenye sukari ya ndani kwani iki jaa nchini itajirekebisha kulingana na mahitaji na upatikanaji wake kwenye soko.
Pili Ramadhani wa mkazi wa Mji mpya mjini hapa alisema serikali imeshindwa kurekebisha soko la sukari ikizingatia kuwa haina uwezo wa kutosheleza mahitaji yay a bidhaa hiyo kwa jamii nakuwa inapaswa kukaa ikiwakutanisha wataalamu wa biashara na uchumi ili kuifanya bei ya sukari kusimama katika soko.
Baadhi ya wafanya biashara wa jumla akiwemo Sadiq Omary na Lucia Kapinga mjini hapa walibainisha kuwa ingawa serikali imetangaza kuingiza sukari lakini bado wanaipata kwa bei ghali hivyo kushindwa kumudu bei elekezi ya serikali katika soko la Jumla .
“tunauziwa kwa kati ya shiingi 94,000 hadi 95,500 unadhani mimi nitauza shilingi ngapi wakati na mimi nauza ili nipate fedha ya kuendeleza biashara na maisha yangu kwa jumla…nadhani serikali inatakiwa kutulia juu ya suala hili la sukari ili iwe na bei inayoendana na hali iliyopo”alisema Omary.
Juhudi za kumpata mkuu wa Mkoa morogoro Dk Kebwe Stephen kuzungumzia changamoto zilizojitokeza hadi bei kuendelea kubaki juu hazikufanikiwa licha ya kutafutwa mara kadhaa ikiwemo kwa simu yake ya kiganjani bila mafanikio baada ya simumu yake kuita mara kadhaa bila kupokelewa.
Hata hivyo mwandishi wa habari hizi anaendelea kumtafuta kwa ufafanuzi Zaidi juu ya changamoto zilizoj






No comments:

Post a Comment