Friday, June 10, 2016

WASICHANA 500 wa tanzania wanatumikishwa kazi za ukahaba

Waziri wa mambo ya nje wa Tanzania  Balozi Augustino Mahigi 
WIZARA ya mambo ya nje nchini Tanzania imesema kuwa zaidi ya wasichana 500 wanatumikishwa kazi za ukahaba katika nchi za Asia na uarabuni.

Msemaji wa wizara ya mambo ya nje nchini Tanzania , Bwana Mindi Kasiga amesema hayo wakati akiongea na wanahabari jijini Dar es salaam hivi karibuni.
Bwana Kasiga amesema kuna mtandao unaowasafirisha wasichana katika nchi hizo kwa madai ya kufanya kazi za ndani lakini baadae hutumikishwa kwenye biashara ya ngono.
Amefafanua kuwa baadhi ya wasichana hao wemekimbilia kwenye ubalozi wa nchi hiyo ili kuomba kurudishwa nyumbani
''

Mtandao huo unachofanya ni pamoja na kuwatafuta wasichana wenye umri kati ya miaka 18 na 24 na hata chini ya umri huo na kuwalaghai kuwa kuna fursa za ajira katika mahoteli, migahawa, maduka makubwa au kazi za nyumbani nchi za nje na kwamba watawasaidia wasichana hao kupata kazi hizo pamoja na kuwawezesha kupata vyeti vya kusafiria VISA na tiketi za ndege kwa ajili ya kusafiri kwenda kwenye nchi husika''.

No comments:

Post a Comment