ASASI ya kutunza mazingira
nchini ya
CONASU yenye makao yake makuu mjini Morogoro ikishirikiana na mfuko
wa kutunza mazingira duniani ‘World wildlife Fund (WWF)zimeanza kurejesha uoto
wa asili ufukweni mwa bahari ya Hindi mashariki mwa Tanzania kwa kupanda mimea
maji jamii ya Mikoko pwani ya mji wa Bagamoyo.
Asasi hiyo inayoungwa mkono pia na halmashauri ya mji huo Mkoani Pwani
inakusudia kupanda eneo lenye jumla ya ukubwa wa hekta nne ukingoni mwa bahari
ya Hindi vikihusishwa vijiji kadhaa kikiwemo cha Mlingotini,Kaole, Kondo na
Pande katika kata ya Saadani,Miono,Kange na Mitipini Wilayani Bagamoyo.
Mkurugenzi wa CONASU Angelus Runji alisema katika
eneo hilo zaidi ya miche 40,000 ya aina mbili za miti hiyo itapandwa ili katika
maeneo yaliyoharibiwa na watu kwa shuguli mbalimbali za kijamii ikiwemo
upasuaji Mbao, Uchomaji mkaa,ujenzi na sanaa ikiwemo uchongaji vinyago na
michezo ya jadi.
“mwaka 2014 tukiwa na mradi wa kupambana na njia haramu za uvuvi na uvuvi
endelevu,tulibaini kupungua idadi ya samaki kutokana na mazalia yao ikiwemo
Mikoko kufyekwa ovyo hivyo samaki kushindwa kuzaliana kwa urahisi na wengine
kupotea kwa kuliwa na samaki wakubwa wengine kufa kwa kushindwa kuishi kwenye
kina kirefu cha maji”alifafanua Runji.
Aidha alisema mbali na Mikoko kuwa na umuhimu kwa mazalia ya samaki pia
mpango wa baadae ni kuanzisha ufugaji Nyuki katika mikoko hiyo mpango ambao
tayari umeanza kutekelezwa kwa baadahi maeneo.
Baadhi viongozi akiwemo mjumbe wa mazingira katika serikali ya kitongoji
cha Kitame Nuru Seif alisema kutoweka kwa mikoko hiyo kwa zaidi ya
miaka 20 iliyopita umewasababishi kuishi maisha duni baada ya kukimbiwa na
waume zao wanakwenda mikoa mingine kutafuta.
Kwa upande wake mwenyekiti wa kitongoji hicho cha Kitame Slvester Kangwe
mbali na kukili kukutoweka kiwango kikubwa cha Samaki na bahari kushindwa
kupumua alibainisha kuwepo ongezeko la kasi ya upepo, gharama ya maisha kupanda
huku takribani wakazi 180 wakikimbia kitongoji hicho chenye takribani wakazi
300.
Waliiomba serikali kuwawezesha kwa elimu ya mazingiri,kuwapatia vifaa vya
ulinzi,Boti kwa ajili ya ulinzi wa ekari hizo 50 za mikoko,mavazi maalumu ya
kuogelea na kuimarisha shuguli za miti hiyo kwa faida ya vizazi vya sasa na
vijavyo kwa kuwakamata na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria wanaohujumu.

No comments:
Post a Comment