Friday, July 22, 2016

JUMAWATA kupanda miti ekari 30 kijiji cha Mtamba, Kisarawe

JAMII ya walemavu imejitoa kimasomaso kwa kushiriki kikamilifu shughuli za  mazingira kwa kujianda na kupanda miti takribani ekari thelathini kuanzia mwezi Disemba mwaka huu.


Mwenyekiti wa Jumuiya ya uchumi  na maendeleo ya walemavu Tanzania (JUMAWATA)Bwana Mshamu Mzanda amebainisha hayo mapema leo wakati akiongea na wanahabari ofisi kwake jijini Dar es salaam.

 Amesema lengo ni kupanda miti ekari hamsini ifikapo machi 2017 katika shamba lao lililopo Mtamba, wilayani Kisarawe , mkoa wa Pwani , lakini wataanza na ekari 30 ili kutekeleza sera ya serikalia ya utunzanji na uhifadhi wa mazingira kwa kupanda miti.

No comments:

Post a Comment