Wednesday, July 20, 2016

LIGI kuu Tanzania Bara kuanza Agosti 17 mwaka huu

LIGI  kuu Tanzania bara msimu wa 2016/2017itaanza kutimua vumbi Agost 20 mwaka huu.
Mchezo wa ufunguzi wa msimu mpya wa ngao ya jamii utachezwa Agosti 17 kwa mabingwa wa msimu uliopita Yanga, kuchuana na Azam waliomaliza katika nafasi ya pili katika msimu wa ligi uliomalizika mwezi Mei.

Michezo rasmi ya ligi hiyo itaanza kupigwa Agosti 20 Kwa Simba SC wakifungua dimba na Ndanda FC Uwanja wa Taifa Dar es Salaam, huku Azam wakiikaribisha African Lyon Uwanja wa Azam Complex,
 Chamazi.Kagera Sugar watacheza na Mbeya City Uwanja wa Kaitaba, Toto Africans watawalika Mwadui FC Uwanja wa CCM Kirumba,Stand United watakua wenyewe wa wageni wa ligi Mbao FC Uwanja wa Kambarage.
Mtibwa Sugar watacheza na Ruvu Shooting Uwanja wa Manungu, Turiani, huku Majimaji na Prisons wakikipiga Uwanja wa Majimaji Songea.Mabingwa watetezi Yanga wataanza mbio za kuutetea ubingwa wao hapo Agosti 31kwa Kuchuana na Jkt Ruvu katika dimba la Taifa Dar es Salaam



No comments:

Post a Comment