JIJI la Dar na Halmashauri zake za Kinondoni, Temeke na Ilala zinakabiliwa
na changamoto ya uhaba wa madampo ya kutupa taka baada ya wananchi wengi kuitikia agizo la
mkoa kufanya usafi kila siku ya jumamosi.
Wakiongea na Mbiu
Media , baadhi ya wananchi wa kata ya Kijichi , manispaa ya Temeke jijini Dar
es salaam wamesema kuwa serikali ya mkoa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali
wa maendeleo hawana budi kuangalia mbinu mbadala za kukabiliana na changamoto
za kukithiri kwa mamdampo madogo madogo yaliyopo mitaani.

No comments:
Post a Comment