![]() |
| Mkuu wa mkoa wa Morogoro Kebwe Steven Kebwe |
WANAKIJIJI
Mngazi,Vigolegole na Milengwelengwe kata na tarafa ya Bwakila chini wilayani
Morogoro wameandamana kupinga vikali kauli ya mkuu wa mkoa huo wa Morogoro
(RC)Dk Stephen Kebwe kuwa wenyeviti wao ndio wanao sababisha migogoro ya
wakulima na wafugaji kwa kuruhusu kiholela uingizaji mofugo katika vijiji
hivyo.
Sambamba na hilo wamemtaka mkuu huyo kuwapelekea tafiti zake na
vielelezo vinavyobainisha wenyeviti hao kuingiza mifugo katika vijiji hivyo
huku wakimtaka Rais Dk John Magufuli kupangua safu ya uongozi mkoa nma wilaya,
jeshi la polisi sambamba na kamati za ulinzi na usalama kwa kufanya kazi kwa
simu badala ya kwenda eneo husika.
Hata hivyo mkuu wa mkoa huo Dk Stephen Kebwe alisema barua za
maelekezo walizotumiwa ni agizo la kitafa katika kushugulikia migogoro hiyo
badala yake kuendelea kuwashutumu baadhi ya wenye viti kukaribisha wafugaji
vijijini nakuwa tayari imetolewa miezi mitatu kuwatambua wavamizi,idadi ya
mifugo na watokako ili uondoshwaji wake uende kwa mujibu wa sheria.
"Barua walizo waonyesha ni maelekezo ya kitaifa kwani katika
uondaji mifugo kunataratibu zake kuepusha changamoto nyingine ikiwemo ya
magonjwa na maelekezo ya sehemu wanapotakiwa kwenda...vinginevyo itakuwa vurugu
isiyo na mwisho"alifafanua Dk Kebwe.
Baadhi yao akiwemo Marium Kibwana,Omary Lukwele na Josephena
Magola kwa nyakati tofauti walisema taarifa hiyo ya(RC) kwenye vyombo vya
habari imewashitua wakiitafsiri kuwa inalengo la kujiwekea kinga ya kutumbuliwa
na Rais kwani tangu viongozi hao akiwemo mkuu huyo wa mkoa wapewe dhamana ya
kuongoza hakuna aliyewahi kuoneka katia vijiji hivyo.
“Walisema wanaamini kuwa mkuu wa mkoa huo ni msomi anyetumia
tafiti na vilelezo kutamka jambo hadharani,hivyo kuomba tafiti na vielelezo
hivyo ili nawao wamwonyesha vielelezo walivyonavyo dhiidi ya wafugaji hao
kuhamia katika vijiji hivyo kisha kulisha mifugo yao kwenye maashamba yao ya
mpunga na mahindi.
“Kama kweli mkuu wa mkoa anauhakika wenyeviti wetu wanaruhusu
mifugo kuingia vijijini basi aondoe taratibu alizoweka za kuondosha mifugo
kisheria aruhusu vijiji viwaondoe wafugaji hata leo! Alisema Josephna Magala.
Walisema chanzo kikubwa cha ongezeko la mifugo vijijini ni vimemo
toka kwa vigogo serikalini na utaratibu mbovu wa kuwafukuza wafugaji unao
tegemea kamati za ulinzi na usalama wilaya na mkoa pekee na kuwa utaratibu huo
umekuwa hautekelezeki kutokana na viongozi ngazi za juu kupuuza kwa kutofanyia
kazi taarifa za viongozi wa vijiji.

No comments:
Post a Comment