Tuesday, August 2, 2016

UKOSEFU wa viwanda vya kusindika nyanya vyachangia kushuka kwa bei ya zao hilo

Mkulima wa nyanya akiwa shambani 
KUKOSEKANA kwa viwanda vingi vya kusindika nyanya nchini ni moja ya changamoto itakayowafanya wananchi wanaojishughulisha na kilimo boiashara kukata tamaa katika sekta ya kilimo.

Hayo yamebainishwa mapema wiki hii na wakulima wa nyanya katika kijiji cha Doma, wilayani Mvomero . mkoa wa Morogoro katika mahojiano na Mbiu Media.
Wamesema kuwa, bei ya nyanya kwa sasa imeshuka na kfikia tenga moja la debe mbili na nusu kuuzwa shilingi elfu tano kutokana na uzalishaji wa zao hilo kuongezeka hali inayosababishwa wakulima kutopata faida stahiki .
Kutokana na na hali hiyo wameiomba serikali ya awamu ya tano kuhakikisha kuwa inakabiliana na changamoto hiyo ili kumuwezesha mkulima kupambana na umaskini wa kipato.


No comments:

Post a Comment