![]() |
| Mkuu wa mkoa wa Morogoro Kebwe Steven Kebwe |
MKUU wa Mkoa
wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe amekerwa na kutelekezwa kituo cha Chazi
wilayani mvomero na kutoa wiki mbili kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya
Mvomero kuingiza maji na umeme kituoni hapo.
Dk. Kebwe alitoa agizo hilo baada ya kusomewa matatizo
yanayokikabili kituo hicho na wazee kisha kujionea hali ya kituo muda mfupi
baada ya kukabidhi zawadi ya vyakula mbalimbali ikiwani mkono wa Iddi kwa wazee
hao kwa niaba ya Rais wa Dk.John Magufuli.
“nimejionea mwenyewe hali ya kituo, sasa hili la maji nampa siku
14 mkurugenzi wa halmashauri awe ameingiza maji hapa haiwezekani mpo karibu na
chanzo cha maji tena ya mseleleko eti hamana maji mimi siwezi kukubali” alisema
Dkt. Kebwe.
Sambamba na agizo hilo alimwagiza Mkurugenzi huyo aliyewakilishwa
na Diana Munywanga kurejesha mara moja Umeme ulikuwepo awali mara baada ya
kukrabatiwa miundombinu yake ikiwemo kuushirikisha uongozi wa Sekondari ya
Sungaji ili kuharakisha upatikanaji umeme huo .
Kuhusu watu waliovamia eneo la kituo hicho cha Kambi ya wazee
lipatalo ekari 1,000, Dkt. Kebwe amewataka wavamizi hao waondoke mara moja
kabla Serikali haijawabomolea nyumba zao, kuwataka walipe gharama za zoezi la
ubomoaji na kuwafikisha mahakamani.
Diwani wa kata ya Sungaji Deoglatias Daniel mbali na shukrani za zawadi hiyo ya rais alisema wazee wengi
wamekuwa hawakai kambini na kuishia mitaani kuomba kutokana na ugumu wa maisha
kambini hapo hivyo kuiomba seriakali kuangalia uwezekano kuwa na bajeti
inayotosheleza mahitaji.
Kituo cha wazee cha Chazi kina eneo lenye ukubwa wa Ekari
3140, Ekari 1000 limevamiwa na wananchi. kina jumla ya Wazee 22 wanaotuzwa
kambini hapo wanawake wakiwa 8 na wanaume 14 na kinakabiliwa na changamoto kubwa
tatu ambazo ni ukosefu wa maji, ukosefu wa vyoo na uhaba wa chakula.
MWISHO.

No comments:
Post a Comment