 |
| Mkuu wa moa Morogoro Kebwe Steven Kebwe |
BAADHI ya wanachi kutoka kata ya
Kolelo wilayani Morogoro wakishirikiana na Diwani wao Erigius Mbena wametua
ofisini kwa mkuu wa wilaya hiyo Regina Chonjo wakimtaka kutoa jibu la hatima ya
migogoro baina yao na kundi la wafugaji lilinaloendelea kukua kila kukicha na
kuwasababishia maafa.
Uamuazi wa kupiga kambi ofisini hapo ulitokana
na wananchi hao wakiwa na baadhi ya majeruhi kati ya 20 waliojeruhiwa karibuni
kufukuzwa ofisi ya Mkuu wa mkoa wakitawalikokwenda kudai hatima ya mapigano
hayo yanyopuuza sheria ndogo za wilaya,vijiji na amri ya mkuu wa mkoa Dk Steven
Kebwe.
“wanachi wamechoshwa na vurugu wanazofanyiwa
wakulima katani mwangu maana kila siku wanapigwa na kujeruhiwa ovyo,watuhumiwa
wakikamtwa hakuna adhabu zozote zinazotolewa dhiidi yao…sasa hapa wanachi
wanataka kupata jibu la wafugaji hao wanaondoka lini basi”alisema Diwani
Erigius Mbena.
Alisema kuchoshwa huko kunatokana kukosekana na
ushirikiano wa utumikaji sheria ndogo za halamashauri,vijiji na maagizo ya
viongozi ikiwemo utozwaji wa faini ya shilingi 20,000 kila mfugo kwa madai kuwa
vyombo hivyo havikushirikishwa wakati wa uandaaji wake wa sheria hizo.
“Tutakuwa hapa hadi tutakapo pata hatima ya tatizo
la migogoro hii ambayo kilasiku sasa inatutia vilema tusivyovitaraji na
kutufanya watumwa kwenye maeneo yetu…tatizo kunakuwafunika wanachi Blanketi la
amani wanachi wakati wamelalia kitanda cha migogoro katika serikali hii ya
awamu ya tano”alisema .
Mkuu wa wilaya hiyo Regina Chonjo alipotafutwa
kutoa ufafanuzi wa tatizo hilo hakuonyesha ushirikiano kwa mwandishi badala
yake baada ya mwandishi kujitambulisha kwake kwa simu ya kiganjani alikata na
kuizima simu hiyo.
Wilaya ya Morogoro iko katika milima ya Urugulu
ambayo jamii yake ni wakulima ambayo katika miaka ya karibuni imeanza kukumbwa
na migogoro ya wakulim na wafugaji na katika kata ya Kolero tayari wameripotiwa
zaidi ya watu 20 kupigwa na kujeruhiwa
No comments:
Post a Comment