WAKULIMA wa viungo , mboga na Nyanya katika kata ya Nyandira wilayani Mvomero, mkoa
wa Morogoro wameitaka serikali kupitia wizara
ya Kilimo na chakula,Mifugo na Uvuvi nchini kupitia wanasayansi na watafiti
kumtangaza mdudu maarufu Kantangaze ‘Tuta absoluta’janga la kilimo kutokana na
kuhatarisha kuteketeza zao hilo nchini.
Hitaji hilo lilitolewa
kwa nyakati tofauti na wakulima wa Nyanya Julius Kobero wa Pinde na Christina
Kibaga wa Kilangali kwenye warsha ya uhamasishaji njia bora ya kuzalisha mazao
hayo kibiashara, tija na masoko iliyoandaliwa na mtandao wa wakulima wadogo
MVIWATA ikishirikiana na Gret ya Ufaransa kwa ufadhili wa Jumuia ya Ulaya EU.
“viungo na mbomboga ndio
zao letu la uchumi tatizo ni mdudu Kantangaze ukweli anatutia umasikini kwa
shambulia na kuharibu mashina,majani na matunda…wanaenea kwa kasi kubwa,
seriakali imtangaze janga na itutafutie dawa ya kumwangamiza vinginevyo
hatutakuwa na nyanya nchini”alisema Christina.
Walisema endapo serikali
itampuuza mdudu huyo ipo hatari kwa wakulima kufilisika na bidhaa hiyo kuwa
kosekana nchini kisha kutegemea kutoka nje ya nchi na vyakula vilivyosindekwa
jambo ambalo ni hatari kwa afya na kiuchumi kwa watanzania.
Awali wakizungumzia
dhamira ya MVIWATA kuwawezesha wakulima hao kuzalisha kwa tija na upatikanaji
masoko na uchumi kukua, mratibu wa mradi huo ujulikanao Malimbichi Ernest
Likoko na Afisa kilimo wa mradi Giovanni Nguvu kwa nyakati tofauti
walibainisha mdudu huyo kuripotiwa serikalini nakuwa tafiti zinaendelea.
“nikweli ndundu huyo
anaweza kutia hasara ya asilimia 100 akiingia kwenye shamba la nyanya kutokana
na kasi kubwa aliyoanayo katika kuzaliana ambapo hutaga zidi ya mayai 260 huku
na kwa mwaka wanazaliana mara Tisa…sasa mdudu mmoja anataga kiasi hicho fikiria
wakiwa 1000 shambani”alisema Nguvu.
Hata hivyo walisema
MVIWATA ikishirikiana na wadau mbalimbali ndani na nje wameanza kutumia mitego
ya asili kuwanasa wadudu majike wa aina hiyo na juhudi zinaendelea kutafuta
njia nyingine kuwakabili wadudu hao ambao ambao wamebainika kutodhulika na sumu
zinazotumika katika mazao hayo.
Kupitia mradi Malimbichi
wenyelengo la kufikia zaidi ya kaya 16,000 na watu 72,000 mkoani Morogoro,
Mviwata inakusudia kuboresha uzalishaji,kupata masoko,ukuzaji uchumi,utunzaji
mazao na mazingira ufanyika katika tarafa nne ikiwemo ya Mgeta kata ya Nyandira
uzalishaji Nyanya,Matombo(Pilipilimanga,ambalasini na karafuu) na Kilolo kata
ya Ruaha mbuyuni(Vitunguu)

No comments:
Post a Comment