JITIHADA za serikali katika kufikia malengo ya milenia ya 2025 huenda yakafanikiwa baada ya asilimia 59 ya kaya nchini kuwa na uhakika wa kupata maji safi na salama, tafiti zimejuza hayo hivi karibuni.
Utafiti uliofanywa na Tanzania HIV/AIDS and Malaria Indicator Survey(THMIS) wa mwaka 2011-2012 kwa kushirikiana na Taasisi ya Takwimu nchini(NBS) umegundua kuwa asilimia 59 ya kaya nchini zina uhakika wa kupata maji safi na salam, ambapo asilimia 44 ya kaya zinatumia zaidi ya dakika 30 kupata huduma maji.
Tanzania ni miongoni mwa nchini zilizosaini mkataba wa Umoja wa Taifa wa mwaka 2002 kuhusu Malengo ya Milenia ikiwemo kuwapatia wananchi kupata maji safi na salama kwa asilimain 100 ifikapo mwaka 2025.
No comments:
Post a Comment