JUMLA ya shilingi million 307 zimekusanywa na jeshi la Polisi kitengo
cha Usalama Barabarani mkoani Iringa kufuatia makosa 10,243
katika kipindi cha miezi mitatu ya Januari hadi Machi mwaka huu.
Akizungumza na waandishi
wa habari ofisini kwake leo kamanda wa polisi kitengo cha usalama
barabarani mkoani humo,B wana Leopord Fungu amesema idadi ya makosa ya
usalama barabarani yameongezeka kutokana na maderava wengi kutofuata sheria
na kusababisha kulipishwa faini.
Bwana Fungu amesema
makosa hayo yameongezeka ukilinganisha na kipindi kama hicho kwa mwaka 2013
kutoka makosa 61,52 hadi makosa 10,243 kwa mwaka huu.
Alisema katika kipindi
cha Januari 1 hadi Machi 31 mwaka 2013 jeshi la polisi kitengo cha
usalama barabarani kilikusanya jumla ya shilingi milioni 185.8 likiwa ongezeko
la shilingi milioni 121.4 kwa kipindi hicho kwa mwaka huu.
Kamanda Fungu ameyataja
baadhi ya makosa hayo kuwa ni makosa ya mwendo kasi , ubovu wa magari,
kutofuata ratiba, kuzidisha abiria, matumizi mabovu ya barabara,kutofunga
mikanda,kubeba mizigo isiyoruhusiwa kisheria,kutovaa helment pamoja na kupakiza
abiria zaidi ya mmoja kwa waendesha pikipiki
No comments:
Post a Comment