IMEELEZWA kuwa zaidi watanzania milioni ishirini na saba wana
simu kadi huku watumiaji wa huduma ya
mtandao (internet)wakiwa milioni tisa nchi nzima.
Hayo yamebainishwa mapema
leo na Naibu mkurugenzi wa masuala ya
watumiaji wa huduma za mawasiliano toka Tume ya mawasiliano nchini (TCRA)Bwana
Isaack Mruma wakati akitoa ufafanuzi kwa waziri wa nchi ofisi ya Raisi
uratibu na mahusiano Mheshimiwa
Steven Wasira wakati akikagua mabanda ya Taasisi na idara mbalimbali za serikali
kwenye maonesho ya Muungano yanaendelea mnazi mmoja jijini Dar es salaam.
Kuhusiana na madai yanayotolewa na watu wengi kuwa amatumizi ya
simu za mkononi yana madhara kwa
watumiaji , Bwana Mruma ameeleza kuwa, mpaka sasa haijathibitishwa kitaaluma na
madai hayo si sahihi kwani Taasisi ya afya Duniani (WHO)imekanusha madai
hayo na kusisitiza kuwa hakuna madhara ya kutumia simu za mkononi sanjari na kuishi jirani na minara ya simu .
No comments:
Post a Comment