Friday, April 18, 2014

TACAIDS yaweka mikakati ya miaka mitano kupunguza maambukizi ya ukimwi



TUME ya Taifa ya kudhibiti ukimwi nchini (TACAIDS) imeweka mkakati wa tatu wa miaka mitano wa  kuhakikisha vifo vitokanavyo na maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi vinapungua na kufikia sifuri ifikapo mwaka 2018.

Afisa sera na mipango kutoka Tume hiyo Bwana Richard Ngurwa ameyasema  hayo jana mjini Morogoro wakati akizungumza na wadau kuhusu utekelezaji wa mpango mkakati wa tatu wa Taifa wa miaka mitano wa kudhibiti ukimwi ambapo amesema pamoja na maambukizi kushuka kutoka asilimia 7.0 hadi kufikia 5.3, bado ipo haja kwa TACAIDS kufikia malengo kwa kuwa na programu maalumu zitakazowawezesha watumishi wa afya kupanga bajeti na kufanikisha malengo hayo.

 Akichangia katika semina hiyo , kaimu katibu Tawala mkoa wa Morogoro Bwana Noel Kazimoto amesema jukumu la kuzuia maambukizi mapya ya virusi vya ukimwi ni la kila raia wa Tanzania bila kujali jinsia,huku mratibu wa TACAIDS mkoa wa Morogoro Nyangusi Laiza,akiwasisitiza wadau kuupa kipaumbele mkakati huo ili kufikia malengo ya Tume hiyo kama yalivyokusudiwa

No comments:

Post a Comment