Friday, April 18, 2014

WATAFITI wa zao la muhogo wapongezwa mkoani Mara



SERIKALI wilaya ya Rorya mkoani Mara imewapongeza watafiti kutoka Taasisi ya  Utafiti wa Kilimo Mikocheni ya jijini Dar es Salaam na Tume ya Taifa ya Sayansi na teknolojia kwa kufanya utafiti katika wilaya hiyo na kupeleka mbegu kinzani za mihogo katika wilaya hiyo. 

Mkuu wa wilaya ya Rorya Mkoani Mara Bw Elias Goloi ametoa pongezi hizo juzi kwa watafiti waliofika wilayani humo kupeleka Mbegu  kinzani  za Mihogo kufuatia utafiti uliofanywa na watafiti hao mwezi February Mwaka huu na kubaini kuoza kwa mbegu za mihogo zilizokuwepo hapo awali.

Amesema kupelekwa kwa Mbengu hizo kutasaidia kuondoa tatizo la kuoza kwa mbegu za Mihogo wilayani humo na kusababisha tatizo la njaa wilayani humo,huku Mkuu wa taasisi ya Utafiti Dr Joseph Ndunguru akisema kuandaliwa kwa Shamba la mfano wilayani humo kutaleta tija kwa wakulima wa wilaya hiyo.

No comments:

Post a Comment