Friday, April 18, 2014

SERIKALI itahakikisha idara ya utafiti inabaki kuwa ya Muungano



SERIKALI imesema kuwa itahakikisha idara ya utafiti inabaki kuwa ni ya Muungano.

Waziri wa sayansi , Teknolojia na mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amebainisha hayo mapema leo  wakati akiongea na waandishi wa habari kwenye maonesho ya Muungano yanayoendelea kwenye viwanja vya mnazi mmoja jijini Dar es salaam.

Profesa Mbarawa amefafanua kuwa wizara ya sayansi na teknolojia ina jukumu la kusimamia na kusambaza ubunifu na teknolojia  mbalimbali  bara na visiwani ili kuboresha maisha ya mtanzania .

Amesema vitu muhimu kwenye mawsiliano ni masafa , ambayo kwa sasa Tanzania bara na visiwani ina namba moja ya masafa iliyopewa na shirika la mawasiliano Duniani (ITU )yenye makao yake makuu Geneva, Uswisi hivyo kama itatokea kuvunja  Muungano itabidi kila nchi iwe na masafa yake.

No comments:

Post a Comment