Saturday, April 19, 2014

WATANZANIA watakiwa kuzitumia fursa za Muungano



WAZIRI mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Mizengo Peter  Pinda amewanasihi watanzania kutumia dfursa zilizopo za muungano ili kujiimarisha kiuchumi na kijamii.

Mheshimiwa Pinda ameyasema hayo leo katika viwanja vya Mnazi momoja wakati akifunga maonesho ya Muungano yaliyoanza siku ya jumatano wiki hii.

Amesema kuwa, ni kweli Muungano unachangamoto zake lakini serikali inachukua hatua mbalimbali katika kukabiliana na changamoto hizo.

Amesema fursa zilizopo ni pamoja upande wa Bara kuwa na idadi ya watu wengi ikiwa na watu milioni arobaini na mbil huku Zanzibar ikiwa na watu milioni moja na laki tatu , hivyo ni muhimu kuzitumia fursa hiziza uwiano wa idadi ya watu katika kupanua wigo wa shughuli za kiuchumi na kijamii katika nchi hizi mbili




No comments:

Post a Comment