Saturday, April 19, 2014

WAHAMIAJI haramu 30 wakamatwa mkoani Kagera



ZAIDI  ya wahamiaji haramu 30 kutoka nchini Burundi wamekamatwa na idara ya uhamiaji mkoani  Kagera baada ya kutoroka kwenye kambi ya wakimbizi iliyoko nchini Uganda na kuingia hapa nchini kinyume cha sheria.

Akitoa taarifa kwa waandishi wa habari hapo jana Afisa uhamiji mkoa wa Kagera George Kombe, amesema kuwa wahamiaji hao haramu  30 walikuwa wakihifadhiwa katika kambi ya wakimbizi ya Nakivale  iliyoko nchini Uganda, lakini walitoroka na kuingia nchini   Tanzania kupitia mpaka wa Bugango  ulioko wilayani Misenyi, na kukamatwa baada ya wananchi kutoa taarifa katika ofisi za uhamiaji.

.

Wakiongea katika mahojiano na Maafisa wa idara ya uhamiaji, baadhi ya wakimbizi hao walipoulizwa kuhusiana na tatizo lililowafanya watoroke katika Kambi hiyo, wamedai kukimbia huduma duni ikiwemo  kutopewa huduma muhimu hasa chakula, hali ambayo inaweza kuhatarisha maisha yao, na kuomba kama kuna uwezekano wa kwenda kambi ya Nyarugusu haupo ,basi wapelekwe kwao Burundi.

No comments:

Post a Comment