WIZARA ya ardhi nyumba
na maendeleo ya makazi imesema hakuna sababu ya wawekezaji
kuhodhi maeneo makubwa ya ardhi pasipo
kuyaendeleza huku wananchi wakiendelelea kuteseka ambapo
serikali inakusudia kuchukua hatua za kuwanyang’anya maeneo hayo
na kuyagawa kwa wananchi wasio na
ardhi ili yaendelezwe kwa shughuli za kilimo .
Naibu
waziri wa Ardhi, nyumba na maendeleo ya
makazi Mheshimiwa George Simbachawene ameyaeleza hayo hivi
karibuni mkoani Morogoro wakati akizungumza na mtandoa wa vikundi
vya wakulima wadogo nchini MVIWATA,ambapo amesema halmashauri
nchini zinatakiwa kufanya kazi kwa uadilifu kusimamia sheria na
mpango wa matumizi bora ya ardhi na kuhakikisha kila mwananchi
anapata fursa ya kumiliki ardhi.
Nae Mkurugenzi
wa mtandao wa vikundi vidogo vya wakulima (MVIWATA) Bwana
Ste Ruvuga amesema wakulima wangependa kuona katiba mpya
inatoa ulinzi na haki katika kumiliki ardhi ili
kupunguza migogoro ya ardhi katika mikoa mbalimbali nchini.
No comments:
Post a Comment