Saturday, April 26, 2014

MKUU wa mkoa wa MOROGORO awataka wananchi na wadau mbalimbali kuwasaidia wahanga wa mafuriko



WANANCHI na wadau katika sekta mbalimbali  wametakiwa kuwasaidia wahanga waliokumbwa na mafuriko katika Mji wa Morogoro na vitongoji vyake. 
Rai hiyo  imetolewa jana na Mkuu wa  Mkoa wa Morogoro Dkt. Joel Bendera alipokuwa akipokea, msaada kwa ajili ya wahanga wa Mafuriko kutoka kwa Kampuni ya Star time na Taasisi ya Islamic Foundation ya Mjini Morogoro,

Aidha Dkt. Joel Bendera amewashukuru Wadau hao kwa Msaada walioutoa kwa wahanga hao wa wafuriko na kuwahakikishia kuwa misaada hiyo  Itawafikia  walengwa kama ilivyokusudiwa

Naye Bi.Zuhur Hanif kutoka kampuni ya Star time na Bwana Ahmed Bawaziri ambaye ni Mwenyekiti wa kamati ya Maafa ya Islamic Foundation,wamesema kuwa wameamua kuungana kwa pamoja ili kuwasaidia wahanga hao kwani wameguswa na matatizo yao na wanatambua mchango wao kwa kiasi  kikubwa katika jamii.

Msaada huo uliotolewa na wadau hao ni unga wa Sembe,Maharage na mafuta ya kupikia vyote vikiwa na thamani ya zaidi ya shilingi milioni mbili.

No comments:

Post a Comment