Saturday, April 26, 2014

MSUYA ampongeza Raisi Kikwete kwa kuanzisha mchakato wa katiba



WAZIRI Mkuu na Makamu wa Rais Mstaafu, Mheshimiwa Cleopa David Msuya amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kwa kuanzisha mchakato wa Katiba Mpya na amemshauri kutokuvunjwa moyo na kile ambacho amekielezea kama “mambo madogo madogo” yanayoendelea ndani ya Bunge Maalum la Katiba.
Aidha, Mzee Msuya amesema kuwa Rais Kikwete hatasahauliwa kwa kipindi chake cha uongozi kutokana na upanuzi mkubwa wa shughuli za maendeleo.
Mzee Msuya mwishoni ameyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati alipozungumza kuwashukuru na kuwaaga wananchi wa Wilaya ya Mwanga, Mkoa wa Kilimanjaro kufuatia hatua yake ya kunga’atuka katika uongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wilayani humo, shughuli ambayo mgeni rasmi alikuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete iliyofanyika ofisi za CCM Wilaya ya Mwanga.
Mheshimiwa Msuya ambaye alishikilia ubunge kwa jumla ya miaka 39, ikiwamo 20 ya Ubunge wa Mwanga na anajulikana kama Baba wa Mwanga.


No comments:

Post a Comment