Wednesday, April 23, 2014

Raisi Kikwete awatka viongozi kutowatumia wananchi katika kufanukisha malengo yao ya kisiasa

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amewataka viongozi nchini kuacha kuwatumia wananchi kama chambo cha kufanikisha malengo yao ya kisiasa na kusababisha migororo na uvunjifu wa amani.
 
Aidha, Rais Kikwete amewataka wananchi wa Wilaya ya Karatu wasiige mfano wa Arusha ambako fujo zinazoongozwa na baadhi ya viongozi zimezorotesha  uchumi wa mji huo kwa sababu usalama ni kigezo kikuu cha maendeleo ya uchumi.
 
Kwa mujibu wa Taarifa ya Mawasiliano ya Rais Ikulu jijini Dar es Salaam,Rais Kikwete ametoa kauli hiyo jana  wakati anazindua Jengo la Halmashauri ya Wilaya ya Karatu, Mkoani Arusha.
Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu, Bw. Lazaro Titus Massey amewaambia wananchi kuwa moja ya mwelekeo mkuu wa CHADEMA wilayani Karatu ni kushirikiana na Serikali na polisi katika kudumisha amani.

No comments:

Post a Comment