Tuesday, April 22, 2014

WAFANYABISHA wa mbogamboga soko la Ilala waikosesha soko mapato



SOKO la Ilala jijini Dar es salaam linakosa mapato kutokana na wafanyabiashara wa mbogamboga kukiuka taratibu na kanuni za uuzaji wa bidhaa kwa kufanya biashara katika mitaa ya Ashanti na Morogoro kinyume na  utaratibu uliowekwa na uongozi wa soko wa kufanya biashara katika viimba maalum.

Hayo yambainishwa mapema leo na mwenyekiti wa soko la Ilala jijini Dar es salaam Bwana Seif Mwera wakati akiongea na mbiu ya maendeleo.

Amesema uongozi wa soko umewasiliana na uongozi wa Halmashauri ya Ilala ili kuwaondoa wafanyabaishara hao lakini Halmashauri imedai kuwa aina fedha ya kuwalipa wanamgambo kwaaajili ya kuendesha zoezi la kuwaondoa wafanyabiashara hao.


No comments:

Post a Comment