Watunukiwa wa tuzo mbalimbali hapa nchini
ambao wanatunukiwa kutokana na michango yao ya kimaendeleo katika jamii wametakiwa
kutoa ushirikiano kwa serikali na jamii
kwa ujumla ili kuleta maendeleo zaidi katika jamii zao.
Wito huo umetolewa hivi karibuni na mkuu wa wilaya
ya Ulanga mkoani Morogoro,Bwana Francis Miti wakati wa utoaji wa tuzo za Ulanga
za mwaka 2013/2014 kwa wanajamii waliotoa mchango wa kimaendeleo katika wilaya
hiyo, tuzo ambazo zimetolewa ili kuhamasisha jamii kushiriki katika shughuli za
kimaendeleo.
Bwana Miti
amesema kuwa licha ya serikali kuthamini michango mbalimbali inayotolewa na
watunukiwa,watunukiwa hao wanapaswa kutoa ushirikiano wa kimaendeleo kwa
wanajamii wengine ili kuweza kuleta maendeleo ya haraka katika jamii zao
Tuzo hizo ambazo zimedhaminiwa na Mahmood international
zimetolewa kwa watu mbalimbali ikiwemo Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Bi Isabela Chilumba kwa usimamizi wa miradi ya maendeleo pamoja na tuzo kwa
wanafunzi waliofanya vizuri mtihani wa
kidato cha nne mwaka jana wakiwa
na mazingira magumu ya kimaisha na kwamba pamoja na kupewa tuzo hizo watasomeshwa
na halmashauri hiyo katika masomo ya kidato cha tano na cha sita.
Jumla ya tuzo kumi na nane za wilaya ya ulanga mwaka 2013/2014
zimetolewa ambazo zimegawanyika katika makundi matatu ya tuzo za heshima,tuzo
za kushindaniwa pamoja na tuzo zinazotolewa na taasisi husika na kwamba hii
ndio mara ya kwanza kutolewa katika wilaya
hiyo.
mwisho.
No comments:
Post a Comment